shuku image TIA MBEYA

Thursday, May 16, 2013

NIGERIAN PROSTITUTES In ITALY

Life Of NIGERIAN PROSTITUTES In ITALY (PHOTOS) What a Shame!!! Why can’t they go back HOME??

WHERE THEY LIVE...

The phenomenon of foreign women, who line the roadsides of Italy, has become a notorious fact of Italian life. These women work in sub-human conditions; they are sent out without any hope of regularizing their legal status and can be easily transferred into criminal networks.
Prostitute waiting for a customer inbraod daylight
 
Many are Africans working as prostitutes to send money home to their families. For nearly twenty years the women of Benin City, a town in the state of Edo in the south-central part of Nigeria, have been going to Italy to work in the sex trade and every year successful ones have been recruiting younger girls to follow them.

Another prostitute chilling at her ''home''
 The Nigerian trafficking industry is fueled by the combination of widespread emigration aspirations and severely limited possibilities for migrating to Europe.The term Trafficking of persons is restricted to instances where people are deceived, threatened, or coerced into situations of exploitation, including prostitution. This contrasts with Human smuggling, in which a migrant purchases services to circumvent immigration restrictions, but it is not a victim of deception or exploitation. More pictures after the cut......
This is where they sleep since they dont have any real home in Italy

 

Most migrant women, including those who end up in the sex industry, have made a clear decision to leave home and take their chances overseas. They are headstrong and ambitious women who migrate in order to escape conflict, persecution, environmental degradation, natural disasters and other situations that affect their habitat and livelihood.


THIS IS WHERE THEY DUMP THEIR CONDOMS AFTER SERVICING THIER CUSTOMERS



Ensuring a better future for one’s family in Nigeria is a principal motivation for emigration within and outside the trafficking networks. Working abroad is therefore often seen as the best strategy for escaping poverty. The success of many Italos, as these women are called, is evident in Edo. For many girls prostitution in Italy has become an entirely acceptable trade and the legend of their success makes the fight against sex traffickers all the more difficult.




One concern is that the anti-trafficking crusade is causing effects opposite to its objectives. What presents itself as a campaign to protect migrants from harm is actually making their efforts to flee home, to find work, to make the most of their lives in often difficult and unforgiving circumstances, much harder.

Wednesday, May 8, 2013

NECTA WAGOMA KUFUTA MATOKEO YA IV, WATISHIA KUJIZURU

NECTA WAGOMA KUFUTA MATOKEO YA IV, WATISHIA KUJIZURU

Prof. Rwekaza Mukandala
WAKATI Serikali ikitangaza kufuta matokeo ya mtihani wa kidato cha nne, Mwenyekiti wa Baraza la Mitihani la Taifa-NECTA ambaye pia ni Makamu Mkuuwa wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Prof. Rwekaza Mukandala amesema hayuko tayari kubadili matokeo ya Kidato cha Nne.

Chanzo cha karibu cha Prof.Mukandala kinadai kuwa mara baada ya kutolewa taarifa ya Serikali inayotaka 'kuboreshwa' kwa matokeo hayo,Prof.Mukandala ameonesha kukataa amri hiyo hadi sasa. 'Sisi tulipitisha matokeo hayo mbele yao na kwa idhini yao.Iweje leo Baraza libadili matokeo?.Tunafanya hivi kwa faida ya nani na kwa ustawi wa elimu ya wapi?' alinukuliwa akihoji Prof.Mukandala.

Habari za kuaminika zinadai kuwa Prof.Mukandala pamoja na Katibu Mtendaji Dr.Joyce Ndalichako wanajiandaa kuachia ngazi kama Serikali itasimamia uamuzi wake huo.

Naye Naibu Waziri wa Elimu na Ufundi Philipo Mulugo alipotafutwa kwenye simu yake ya mkononi kuzungumzia suala hilo iliita bila ya kupokelewa na baadaye akatuma ujumbe mfupi akisema, "Sorry I'm busy call back later", alisema Mulugo kupitia simu yake ya mkononi.

ALCHOKISEMA KARDINAL PENGO KUHUSU BOMU LILILOPIGWA KANISAN ARUSHA ASEMA AMEPATA TAARIFA KUTOKA KWA WATU AMABO HANA SHAKA NAO.

ALCHOKISEMA KARDINAL PENGO KUHUSU BOMU LILILOPIGWA KANISAN ARUSHA ASEMA AMEPATA TAARIFA KUTOKA KWA WATU AMABO HANA SHAKA NAO.


Kadinali Pengo

Dar es Salaam/Arusha. Kadinali Pengo alisema amepata taarifa kutoka kwa watu ambao hana na shaka nao.


“Jana (juzi), niliongelea kwamba suala zima la tukio la Arusha halihusiani na imani yoyote ya kidini. Tamko hilo nilitamka kutokana na taarifa nilizofikishiwa na watu ambao sikuweza kuwa na shaka kwamba wanaoniambia ni kweli na sidhani kama ningekuwa na sababu ya kusema wamefika kwa kunidanganya kwa hiyo tamko litakuwa limesimama juu ya msimamo huo,” alisema Kadinali Pengo na kuongeza:


“Lengo la msingi kabisa, langu na la kanisa ni kwamba tukio lolote lile liwe kwa nia mbaya au nzuri kwa upande wetu isiwe ni sababu ya kuanza mapambano na kuwa chimbuko la ukosefu wa amani katika nchi yetu,” alisema Pengo.


Alisema kuwa kila anayehusika ajue amani ya kweli ya taifa lolote haiwezi ikapatikana isipokuwa ikijengwa juu ya ukweli na ukweli kabisa bila kufuta au kujaribu kupotosha ukweli kwa namna yoyote ile.


“Tusipojua kusema ukweli ulivyo hatuwezi kufaulu kuleta amani katika taifa letu. Kwa hiyo pamoja na kuendelea kuwaomba waumini wa Katoliki pamoja na watu wenye mapenzi mema kuendelea kumwomba Mwenyezi Mungu arehemu taifa letu na mapambano ya aina yoyote ile. Tuendeleze nia yetu njema ya kusema ukweli, haidhuru ukweli huu unamgusa nani,” alisema Pengo.



Alisema kujaribu kuficha ukweli na kupotosha ni njia sahihi kwa ibilisi kuleta vurugu katika jumuiya ya watu na ieleweke hivyo.


“Naomba kila mtu akubaliane na tamko langu haidhuru pana kosa, amani ya taifa letu ni jambo la msingi na amani itajengwa tu iwapo kila mtu anayehusika atakuwa tayari kusema ukweli kama ulivyo,” alisema.


Mwingine afariki, 20 wakutwa na vipande vya chuma miilini


Katika hatua nyingine, majeruhi mmoja katika shambulio hilo lililotokea Jumapili iliyopita, amefariki dunia juzi jioni na kufikisha idadi ya waliopoteza maisha kufikia watatu.


Aliyefariki ni mtoto wa miaka tisa, Patricia Joachim ambaye alikuwa amehamishiwa Hospitali ya Rufaa ya KCMC, Moshi. Wengine waliofariki katika tukio hilo ni Regina Losyoki (45) na James
Gabriel (16).


Mazishi ya watu hao watatu yamepangwa kufanyika katika eneo la kanisa hilo Ijumaa.


Katika hatua nyingine, majeruhi 20 wamebainika kuwa na chembechembe za vyuma walivyopata katika shambulio hilo. Hao ni miongoni mwa majeruhi 42 waliolazwa hadi sasa kwenye hospitali mbalimbali za Arusha.


Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mount Meru, Dk Thomas Kway alisema majeruhi hao 20 wamedhuriwa na chembechembe za vyuma vya mabomu na baada ya miili yao kubainika kuwa na vyuma vyenye urefu hadi wa sentimita tisa.


Dk Kway alisema hayo wakati Waziri Mkuu, Mizengo Pinda alipofika katika hospitali hiyo kuwafariji majeruhi hao.


Kutokana na hali hiyo, Pinda aliwataka madaktari waliowafanyia upasuaji majeruhi waliolipuliwa na bomu kuhifadhi vipande hivyo ili vitumike katika uchunguzi.


Aliwaambia wabunge kuwa vyuma hivyo vitasaidia upelelezi ili kufahamu aina ya bomu lililotumika.


“Tumeamua kuwa vipande vya vyuma vinavyotolewa baada ya upasuaji visitupwe, vitumike kwa uchunguzi,” alisema Pinda na kuongeza kuwa baadhi ya majeruhi wamepelekwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa matibabu zaidi.


Waliokamatwa


Akitoa taarifa kwa Rais Jakaya Kikwete ambaye alifika Arusha jana, Mkuu wa Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo alisema watu tisa wamekamatwa hadi sasa.


Aliwataja baadhi yao kuwa ni Victor Ambrose na wengine aliowataja kwa jina mojamoja ni Joseph na David.


Alisema wengine ni raia watatu wa Saudi Arabia, ambao walikuwa na wenyeji wao wawili na Watanzania wengine watatu.


Kauli ya Kikwete


Akizungumza Arusha jana, Rais Kikwete amewataka waumini wa dini zote waendelee kusali akiahidi kwamba Serikali itaimarisha ulinzi. Alisema amekerwa na kukasirishwa na tukio hilo
.
Rais Kikwete alitanguliwa kufika Arusha na Makamu Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Shariff Hamad na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Idd ambao pia walitembelea Kanisa lililolipuliwa na baadaye kwenda kuwatembelea wafiwa na kuwafariji majeruhi hospitali.


Viongozi wote hao walitoa wito kwa Watanzania kulinda amani iliyopo na kuacha malumbano ambayo hayana tija kwa maslahi ya taifa.