shuku image TIA MBEYA

Sunday, May 13, 2012

Wanaharakati Wakemea Vitisho Kwenye Mchakato Wa Katiba




TAMKO DHIDI YA VITISHO, VIKWAZO NA VITENDO VYA VIONGOZI
VINAVYOTIA WANANCHI HOFU KATIKA KUSHIRIKI MCHAKATO WA KATIBA
MPYA TANZANIA

Jukwaa la Katiba Tanzania na Baraza la Katiba Zanzibar tumeendelea
kufuatilia maandalizi ya mchakato wa kuandika Katiba mpya ikiwa ni
pamoja na kuteuliwa na kuapishwa kwa Tume ya Katiba; Hotuba mbalimbali
za viongozi wa kitaifa kuhusiana na mchakato wa Katiba mpya pamoja na
mwitikio wa wananchi kwa ujumla.

Kwanza, tunawapongeza wote walioteuliwa kulitumikia taifa letu kama
wajumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba Tanzania. Kwa maoni yetu, Tume
iliyoteuliwa imesheheni watu wenye sifa, uwezo na uweledi mkubwa kiasi
kwamba kama itazingatia misingi mikuu ya uundaji wa Katiba Mpya na ya
Kidemokrasia inaweza kufanya kazi hiyo vizuri sana. Kwa madhumuni ya
kujikumbusha, baadhi ya misingi hiyo ni ushiriki mpana wa wananchi,
usikivu na ukusanyaji maoni unaozingatia uhuru kwa kila mtanzania
kutoa maoni yake bila kukwazwa, kuzuiwa au kutishiwa. Hata hivyo
tumesikitishwa   .... Soma zaidi:

No comments:

Post a Comment